1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Pigo kubwa kwa al-Qaeda Afrika Mashariki

13 Juni 2011

Kiongozi wa tawi la al-Qaeda katika Afrika Mashariki aliuawa tangu katikati ya wiki iliyopita, lakini ni siku ya Jumamosi ndio alipotambuliwa kwa hakika kuwa huyo ni Fazul Abdullah Mohammed.

https://p.dw.com/p/RTFW
epa02775194 (FILE) An FBI handout picture dated 26 May 2004 shows Fazul Abdullah Mohammed, the alleged mastermind behind the 1998 terrorist attacks on US embassies in Kenya and Tanzania. Fazul Abdullah has been killed at a roadblock in Mogadishu, Somalia, on 08 June 2011, according to Somali and Kenyan officials, the Somalia Report said on 11 June. Fazul, who has numerous aliases, was reportedly the leader of al-Qaeda operations in East Africa and top military commander of al-Shabaab, the Islamist militant insurgent group engaged in a bid to control Somalia. EPA/FBI / HANDOUT B/W ONLY HANDOUT EDITORIAL USE ONLY +++(c) dpa - Bildfunk+++
Kiongozi wa al-Qaeda Afrika Mashariki, Fazul Abdullah Mohammed alieuawa SomaliaPicha: picture-alliance/dpa

Kwanza aliuawa Osama bin-Laden na sasa ni kiongozi wa al-Qaeda katika Mashariki ya Kati. Marekani imesherehekea kifo cha Fazul Abdullah Mohammed kama pigo kubwa dhidi ya mtandao wa kigaidi. Kwa miaka kadhaa, kiongozi huyo wa ugaidi aliweza kujificha na mara kwa mara alikwepa kukamatwa akitumia majina mavazi tofauti. Safari hii alipigwa risasi na kuuawa, baada ya kusimamishwa kwa bahati tu, kwenye kituo cha ukaguzi barabarani, nchini Somalia. Afisa wa serikali ya Marekani amesema, sasa kundi la al-Qaeda limepoteza kiongozi mwenye ujuzi mkubwa wa kupanga operesheni za mtandao huo.

Ausschnitt aus: ** FILE ** A FBI most wanted poster of Fazul Abdullah Mohammed who has been indicted by a U.S. Feberal court for his involvement in the 1998 U.S. embassy attacks in Kenya and neighboring Tanzania, displayed on the FBI's website Friday, March 21, 2003. Mohammed a senior al-Qaida suspect was reported killed by the recent U.S. air strikes in Somalia. Abdirizak Hassan, the Somali president's chief of staff, told The Associated Press Wednesday Jan. 10, 2006 that Somali leaders had received a U.S. report that included a claim that "that Fazul Abdullah Mohammed is dead." At least three U.S. airstrikes have been launched in the country, Hassan added. (AP Photo)
Fazul Abdullah Mohammed aliesakwa tangu mwaka 1998Picha: AP

Ukweli ni kwamba kundi hilo la kigaidi, limedhoofika kutokana na kifo cha Fazul Abdullah Mohammed aliekuwa na umri kama miaka 40. Yeye alikuwa mwerevu, mtaalamu wa compyuta, alizungumza lugha tano kwa ufasaha na yeye ndiye aliepanga shambulio la kwanza kabisa la al-Qaeda. Hata kabla ya mashambulizi ya Septemba 11 mwaka 2001, kundi hilo la kigaidi mnamo mwezi wa Agosti mwaka 1998, lilishambulia kwa wakati mmoja, balozi za Marekani nchini Tanzania na Kenya.

Mashambulio hayo yalisababisha vifo vya takriban watu 240. Kuanzia hapo, Fazul Abdullah Mohammed alikuwa katika orodha ya watu wanaosakwa zaidi.

Kufuatia kifo cha Osama bin-Laden, ilichukuliwa kuwa yeye ndio atakaerithi nafasi yake. Inasemekana kuwa wote wawili walikuwa na heba. Wale waliokuwa karibu nao, wamewaeleza kama watu waliokuwa wema, waliotulia na waliokuwa na vipaji vya kuvutia watu.

Na kwa mtandao wa al-Qaeda, Fazul Abdullah Mohammed alikuwa muhimu sana kwani aliweza kuwavutia wafuasi wapya. Yeye alitayarisha kambi za kutoa mafunzo kwa washambuliaji vijana nchini Somalia na aliweza kuwasadikisha kuwa ni sahihi kujitoa mhanga kwa Mwenyezi Mungu. Sasa, tawi la al-Qaeda katika Mashariki ya Kati limeachwa na pengo.

Lakini mtandao wa al-Qaeda hauna shida ya kupata wafuasi wapya, kwani nchini Somalia kuna maelfu ya wanaume vijana, wasiojua chochote isipokuwa vita na wao wapo tayari kujitoa mhanga.

Mwandishi: Diekhans,Antje,ZPR

Mhariri:Miraji Othman