1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Polisario kuendeleza mapambano ya silaha

15 Desemba 2007
https://p.dw.com/p/CbxN

ALGIERS

Kiongozi wa chama kinachogombania uhuru wa Sahara Magharibi amesisitiza haja ya mapambano ya silaha dhidi ya Morocco.

Katibu Mkuu wa chama cha Polisario Mohamed Abdelaziz ameauambia mkutano mkuu wa siku tano wa chama hicho ulioanza hapo jana katika eneo linalogombaniwa kwamba wanaendesha vita vya ukombozi ambavyo vitaendelea hadi hapo yatakapofanikiwa malengo yaheshima.

Ameongeza kusema kwamba azimio la kimataifa linahalalisha mapambano yao ya kutetea haki zao kwa kutumia njia zozote zinazowezekana kwa upinzani wa amani na kwa mapambano ya silaha.