1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Polisi Tanzania yalaumiwa kuwahangaisha waandishi habari

Isaac Muyenjwa Gamba10 Agosti 2018

Jeshi la polisi nchini Tanzania linaripotiwa kuwazuia waandishi wa habari kufanya kazi zao kando na kutumia nguvu zaidi dhidi ya baadhi ya waandishi wa habari.

https://p.dw.com/p/32xCo

Hivi karibuni mwandishi mmoja wa habari wa gazeti la Tanzania Daima aliripotiwa kupigwa na maafisa wa polisi Kanda maalumu ya polisi Tarime mkoani Mara wakati akiwa katika majukumu yake ya kazi na August 8 mwaka huu katika mchezo wa kirafiki wa Simba na Kilabu ya Asante Kotoko mwandishi wa habari Silasi Mbise anaripotiwa pia kupigwa na maafisa wa polisi wakati akiwa katika majukumu yake ya kazi. Isaac Gamba amezungumza na Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari nchini Tanzania Kajubi Mukajanga kutaka kujua wamepokea vipi matukio hayo dhidi ya waandishi habari.