1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais wa Brazil hatimaye ajitokeza

22 Juni 2013

Rais wa Brazil Dilma Rousseff amemaliza ukimya aliokuwa nao juu ya maandamano makubwa ya ghasia, akisema kuwa maandamano ya amani ni sehemu ya demokrasia imara lakini ghasia haziwezi kuvumilika.

https://p.dw.com/p/18uJX
Brazilian President Dilma Rousseff delivers a speech during a ceremony at Planalto Palace in Brasilia, on June 18, 2013. Rousseff said Tuesday that the voices of the hundreds of thousands of youths protesting across Brazil over the huge cost of hosting sporting events like the World Cup must be heard. AFP PHOTO / Evaristo SA (Photo credit should read EVARISTO SA/AFP/Getty Images)
Rais wa Brazil Dilma RousseffPicha: E.Sa/AFP/GettyImages

Ameahidi  kuimarisha  huduma  za umma  na  kufanya  mazungumzo na  viongozi  wa  maandamano.

Lakini  bado  haifahamiki  hasa  nani  anaweza  kuwakilisha  makundi makubwa  ambayo  hayana  uongozi  ya  waandamanaji  wanaoingia mitaani, wakitoa  hasira  zao  dhidi  ya  huduma  mbovu  za  umma licha  ya  mzigo  mkubwa  wa  kodi  unaowakabili.

RIO DE JANEIRO, BRAZIL - JUNE 20: Protestors display banners during the FIFA Confederations Cup Brazil 2013 Group B match between Spain and Tahiti at the Maracana Stadium on June 20, 2013 in Rio de Janeiro, Brazil. (Photo by Ronald Martinez/Getty Images)
Waandamanaji wakionesha bangoPicha: Getty Images

"Nitakutana  na  viongozi  wa  maandamano  ya  amani, nataka taasisi  ambazo  ziko  wazi zaidi , zinaopinga  matendo  mabaya," Rousseff  amesema  akimaanisha  hisia  za  rushwa  katika  siasa za  Brazil,  hali  ambayo  inajitokeza  kama  lengo  la  maandamano hayo. "Raia  wake  na  sio  uwezo  wa  kiuchumi  ndio  unapaswa kuwa  mbele."

Waandamanaji  wanataka huduma bora

Licha  ya  kuwa  hakutoa  maelezo  zaidi , Rousseff  amesema  kuwa serikali  yake  itatengeneza mpango  maalum  wa  kitaifa  kwa  ajili ya  usafiri  wa  umma  katika  miji, kupanda  kwa  nauli  za  mabasi na  treni  za  mijini  lilikuwa  ni  lalamiko  la  msingi  la waandamanaji.

RIO DE JANEIRO, BRAZIL - JUNE 20: Protestors display banners during the FIFA Confederations Cup Brazil 2013 Group B match between Spain and Tahiti at the Maracana Stadium on June 20, 2013 in Rio de Janeiro, Brazil. (Photo by Alexandre Loureiro/Getty Images)
Maandamano yakiendelea mjini RioPicha: Getty Images

Pia  amerudia  uungaji  wake  mkono  wa  mpango ulioko  katika  bunge  la  nchi  hiyo  kuwekeza  mapato  yote  ya mafuta  katika  elimu  na  ahadi  aliyoitoa  hapo  kabla  ya  kuwaleta madaktari  kutoka  nje  katika  maeneo  ambayo  yanakosa waganga.

Kiongozi  huyo  ambaye ni muasi  wa  zamani  wa  kundi  la kikomunist  ambaye  amepambana  dhidi  ya  utawala  wa  kijeshi  wa Brazil  mwaka  1964  hadi  1985 na  alifungwa  kwa  muda  wa miaka  mitatu  na  kuteswa  na  utawala  huo  wa  kijeshi, ameelezea kuhusu alivyojitolea  muhanga  hapo  kabla  kulifanya  taifa  hilo kuwa  huru  kutokana  na  utawala  wa  kidikteta.

A demonstrator holds a sign that reads, "Brazil, a country of theft," during an anti-government protest in Porto Alegre, southern Brazil, June 20, 2013. Tens of thousands of demonstrators marched through the streets of Brazil's biggest cities on Thursday in a growing protest that is tapping into widespread anger at poor public services, police violence and government corruption. REUTERS/Gustavo Vara (BRAZIL - Tags: CIVIL UNREST POLITICS BUSINESS EMPLOYMENT SPORT SOCCER)
Mwandamanaji akibeba bango linalosema "Brazil nchi ya wezi".Picha: Reuters

"Kizazi  changu  kilipambana   mno  ili sauti  katika  mitaa  ziweze kusikika," Rousseff  amesema . "Wengi  walishtakiwa, waliteswa  na wengi  wameuwawa  kwa  ajili  hiyo. Sauti  za  mitaani  ni  lazima zisikike  na  kuheshimiwa  na zinaweza  kufikiriwa  vibaya  kwamba ni  kelele  na  ghasia  za  baadhi  ya  watu  wanaopenda  kufanya ghasia.

Akosolewa

Amekosolewa kwa kiasi kikubwa kwa kutoonekana na kujali   huku maandamano yakifanyika na kushindwa kuhusika  na  jamii ambayo inadai serikali yake iwasikilize.

Edvaldo Chaves , mwenye  umri  wa miaka  61 mlinzi wa nyumbani katika  kitongoji  kinachokaliwa  na watu  wenye uwezo kiasi cha  Flamengo mjini Rio, amesema ameiona hotuba aliyotoa Rousseff siku ya Ijumaa kuwa inaridhisha.

"Nafikiri  alikuwa  mtulivu  na  alifanya  kazi  nzuri. Pamoja  na kwamba , kwasababu  alikuwa  mpiganaji  na  aliishi  uhamishoni , anazungumzia  masuala  ya  waandamanaji  kwa  uhakika  zaidi," Chaves  amesema. "Nafikiri  mambo  yatatulia  sasa. Huenda tutaendelea  kuwaona  watu  mitaani  lakini  huenda  itakuwa  ni idadi  ndogo.

Mwandishi:  Sekione  Kitojo / ape

Mhariri: Bruce Amani