1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

SACRAMENTO : Steinmeir yuko California

30 Agosti 2007
https://p.dw.com/p/CBUR

Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeir amewasili katika jimbo la Carlifonia nchini Marekani kwa mazungumzo na gavana wa jimbo hilo Arnold Schwarzenegger.

Mkutano wao katika mji mkuu wa jimbo hilo Sacramento unatagemewa kulenga mabadiliko ya hali ya hewa na uwezekano wa kuratibu mabadilishano ya mifumo ya utowaji wa gesi zenye kuathiri mazingira barani Ulaya na Marekani.