1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

SAO PAULO.Mama aliyemwuua mtu aliyembaka mwanawe achiwa huru

15 Novemba 2006
https://p.dw.com/p/CCsb

Mama mmoja aliemwuuwa mtu aliembaka mtoto wake wa kiume ameachiwa huru nchini Brazil.

Mahakama ya mjini Sao Paulo imepitisha uamuzi huo kwa kueleza kwamba mwanamke huyo bibi Maria do Carmo Ghislotti alimwuua mbakaji huyo ili kutetea haki ya mwanawe mwenye umri wa miaka mitatu.

Bibi Maria Ghilotti alimwuuwa mhalifu huyo kwa kutumia sime.