1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Serikali ya Yemen na waasi watia saini makubaliano ya amani

Sekione Kitojo
6 Novemba 2019

Serikali ya  Yemen inayoungwa  mkono  na  Saudi Arabia  na waasi wa kusini  wanaotaka  kujitenga wametia  saini makubaliano jana kumaliza mvutano  wa  kuwania  madaraka  katika  eneo  la kusini  ya  Yemen.

https://p.dw.com/p/3SX8p
Saudi-Arabien Riad | Einigung auf Friedensplan im Jemen
Picha: Reuters/Saudi Press Agency

Mrithi wa ufalme wa  Saudi Arabia ameyasifu kuwa  makubaliano hayo  kuwa  ni  hatua  kuelekea  suluhisho  pana la  kisiasa  na kuweza  kumaliza mzozo  huo wenye  ncha nyingi. 

Mkwamo  ulifungua  eneo  lingine  katika  vita  vya  zaidi  ya  miaka minne  na  kutia  ufa  katika  muungano  unaoongozwa  na  saudi Arabia  unaopigana  na  vuguvugu  la  Wahouthi  ambalo  liliiondoa serikali  inayoongozwa  na  rais Abd-Rabbo Mansour Hadi  kutoka mji  mkuu , Sanaa, upande wa  kaskazini  mwa  nchi  hiyo mwishoni mwa  mwaka  2014.

Saudi-Arabien Riad | Einigung auf Friedensplan im Jemen
Mwanamfalme mteule wa Abu Dhabi Sheikh Mohammed bin zayed al-Nahyan, (kushoto)na rais Abd-Rabbu mansour Hadi na mwanamfalme mteule wa Saudi Arabia Mohammed bin Salman (kulia)Picha: Reuters/Saudi Press Agency

Balozi  wa  Saudi Arabia  nchini  Yemen  aliwaambia  waandishi habari  kuwa  makubaliano hayo , yaliyofikiwa  baada  ya  zaidi  ya mwezi  mmoja  wa  mazungumzo  ya  ana  kwa  ana  katika  mji  mkuu wa  Saudi Arabia , utashuhudia  kundi  hilo  linalotaka  kujitenga  la kusini  mwa  Yemen linalojulikana  kama  Southern Transitional Council, STC, likijiunga  na  baraza  jipya la  mawaziri  pamoja  na watu  wengine  wa  kusini  na  makundi  yote  yenye  silaha yatawekwa chini  ya  udhibiti wa  serikali.

Mwanamfalme Mohammed bin Salman alisema.

"Makubaliano  haya  yatafungua , uaminifu, mazungumzo  mapana kati ya  makundi  ya  Wayemeni  ili  kufikia suluhisho  la  kisiasa ambalo litafikisha  mwisho  mzozo  huu  wa  Yemen na  kuilinda Yemen, pamoja  na  kila  kitu  kilichomo, dhidi ya  wale  ambao hawaitakii  mema. tunamuomba  Mungu abariki juhudi  zetu na  kuona kuwa  zinafanikiwa, kwa  ajili  ya  nchi  zetu  na  watu  wetu."

Mwanzo mzuri

Rais  wa  Marekani Donald Trump ameyasifu  makubaliano  hayo kupitia  ukurasa  wa  Twitter kwa  kusema , "Mwanzo mzuri sana ! tafadhali  fanyeni kazi wote  kupata  makubaliano ya  mwisho."

Saudi-Arabien Riad | Einigung auf Friedensplan im Jemen
Wawakilishi wa serikali ya Yemen na wapiganaji wanaotaka kujitenga kusini mwa Yemen wakitia saini makubaliano hayo.Picha: Reuters/Saudi Press Agency

Saudi Arabia  imekuwa  ikijaribu  kutatua  mkwamo  huo  katika kuweka  mwelekeo  mpya kwa  muungano  unaopambana  na vuguvugu  la  wahouthi  linaloungwa  mkono  na  Iran katika  mpaka wa  kusini.

Majeshi  yanayotaka  kujitenga , yakisaidiwa  na  mshirika  muhimu wa  Saudi Arabia , Umoja  wa  Falme za  Kiarabu, ni  sehemu ya muungano  wa  Waislamu  wa  madhehebu  ya  Sunni  ambao umeingilia  kati  nchini  Yemen  Machi mwaka  2015 dhidi  ya Wahouthi  ambao  wanaushikilia  mji  mkuu  wa  Sanaa pamoja  na mingi  ya  miji  mikubwa.

Lakini  kundi  la  STC , ambalo  linataka  utawala  wa  ndani  katika eneo  la  kusini  na  kuwa  na  sauti  katika  Yemen  ya  hapo baadae, limeigeuka serikali  ya  Hadi mwezi Agosti, na  kukamata  mji wake mkuu wa  bandari ya  kusini  ya  Aden na  kujaribu  kupanua himaya  yake  upande  wa  kusini.