1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Shambulio katika kanisa nchini Nigeria

6 Januari 2012

Wakati baadhi ya raia wa Nigeria wakiendelea kuomboleza kufuatia vifo vya zaidi ya watu 40 walioshambuliwa mwishoni mwa mwaka jana na kundi la Boko Haram, tukio kama hilo limejirudia tena usiku wa kuamkia leo.

https://p.dw.com/p/13fE6
Onlookers gather around a car destroyed in a blast next to St. Theresa Catholic Church in Madalla, Nigeria, Sunday, Dec. 25, 2011. An explosion ripped through a Catholic church during Christmas Mass near Nigeria's capital Sunday, killing scores of people, officials said. A radical Muslim sect claimed the attack and another bombing near a church in the restive city of Jos, as explosions also struck the nation's northeast. (Foto:Sunday Aghaeze/AP/dapd)
Mashambulio nchini NigeriaPicha: dapd

Ikiwa ni juma moja tu tangu kutokea kwa mkasa huo uliosababisha vifo vya zaidi ya watu 40, kumetokea shambulio lingine jijini Gombe na kupotea maisha ya waumini sita wa dini ya Kikristo.

Kwa mujibu wa taarifa ya serikali ya Rais Goodluck Jonathan, shambulio hilo liliotokea usiku wa kuamkia leo limewajeruhi watu wengine kumi.

Tukio hilo limeshuhudiwa katika mji wa kaskazini mashariki mwa Nigeria, siku chache tu baada ya mabomu mawili kulipuliwa jijini Maiduguri na Damaturu.

Akielezea mkasa huo, Ofisa mmoja wa kanisa la Deeper Life Church,  Ishaya Bako, ameliambia Shirika la Habari la Ujerumani kuwa anaamini wapiganaji hao waliovamia waumini wa kanisa hilo ni wafuasi wa kundi la Kiislam la Boko Haramu.

Wapiganaji hao waliokuwa na silaha kali walishambulia kanisa hilo wakati ibada ikiendelea na kuwafyatulia risasi waumini, tukio lililomuua pia mke wa mchungaji wa kanisa hilo.

Wapiganaji hao walilishambulia kanisa katoliki la mjini Madala, siku ya mkesha wa Noeli na kuua watu ishirini na sita, papo hapo.

Boko Haram ni kundi la Kiislamu ambalo linaishinikiza serikali ya Nigeria itumie sheria za kiislamu, wito ambao unapigwa vita na wengi, hususan waumini wa kikristo.

Bystanders gather around a burned car outside the Victory Baptist Church in Maiduguri, Nigeria, Saturday, Dec. 25, 2010. Authorities say dozens of assailants attacked the church on Christmas Eve, killing the pastor, two members of the choir and two people passing by the church. Police are blaming members of Boko Haram, a radical Muslim sect. (AP Photo - Njadvara Musa)
Kikundi cha Boko Haram ndicho kinachohusika na mashambulizi nchini NigeriaPicha: APImages

Wakiendelea na kampeni hiyo, viongozi wa Boko Haram walitoa sharti la mwisho kwa wakristo, kuhakikisha wanahama kutoka eneo la Kusini mwa nchi hiyo. Waumini hao walipewa siku tatu kutimiza sharti hilo na muda huo uliisha siku ya Jumatano.

Wakazi hao wa eneo la kusini, ambao wengi wao ni wakristo hawakutilia maanani sharti hilo, na baadhi yao wakaona ni kitisho.

Licha ya Rais Goodluck Jonathan kutangaza hali ya hatari, kundi la Boko Haram linaendelea kusababisha kizaazaa nchini Nigeria, hali inayozua maswali mengi ya kwa nini wapiganaji hawa hawadhibitiwi, ilhali serikali hiyo ina majeshi.

Mwandishi: Pendo Paul\dpa

Mhariri:  Othman, Miraji