1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Orodha ya wagombea wa uongozi wa FIFA

26 Oktoba 2015

Sheikh Salman, mwenyekiti wa shirikisho la kabumbu barani Asia amejiunga na orodha ya wagombea wengine watano waliojitokeza hadi sasa kupigania wadhifa wa zrais wa FIFA

https://p.dw.com/p/1GuUU
FIFA Salman Bin Ibrahim Al Khalifa
Picha: picture-alliance/dpa/P. B. Kraemer

Upande wa wagombea wazito wazito anakutikana Michel Platini, aliyesitishiwa kwa muda shughuli zake na Tokyo Sexwale wa Afrika Kusini. Wengine watatu waliosalia wanaonekana kana kwamba hawana nafasi kubwa ya kufanikiwa.

Bado kuna muda lakini hadi saa sita za usiku wa leo kuamkia kesho Jumanne,wakati daftari la maombi litakapofungwa.Orodha ya wanaoomba kugombea wadhifa huo inaweza kuwa ndefu hadi wakati huo na matokeo ya uchaguzi wa atakaemrithi Blatter, February 26 mwakani, hayakadiriki.Mbali na wagombea hao watatu tuliowataja,wengine ni pamoja na Mwanamfalme Ali wa Jordan,Jérome Champagne wa ufaransa na David Nakhid wa Trinidad.

Mwandishi:Hamidou Oummilkheir/SID
Mhariri: Gakuba Daniel