1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Soka. ManU waangukia pua.

5 Aprili 2007
https://p.dw.com/p/CCCS

Katika michezo miwili ya duru ya kwanza ya michezo ya robo fainali katika kinyang’anyiro cha kombe la mabingwa la vilabu barani Ulaya , jana jioni kumekuwa na michezo miwili. As Roma ya Italia imeigaragaza Manchester United ya Uingereza kwa mabao 2-1 wakati Valencia ya Hispania ikiwa ugenini imeilazimisha Chelsea ya Uingereza kutoka sare ya bao 1-1 katika uwanja wa Stanford Bridge.