1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Tanzania inaweza kujifunza nini kutoka kwa Kenya?

Elizabeth Shoo21 Oktoba 2015

Baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007, Kenya ilishuhudia machafuko. Tanzania inaweza kujifunza kutokana na makosa ya nchi hiyo jirani ili kuhakikisha amani inatawala, wanasema wachambuzi.

https://p.dw.com/p/1GrXt
Vurugu baada ya uchaguzi mkuu Kenya 2007
Picha: Getty Images

Wakati hali ikionekana kuwa shwari kuelekea uchaguzi mkuu tarehe 25 Oktoba, kuna wasiwasi pia unaojitokeza wa kutokuwepo hali nzuri ya usalama nchini Tanzania wakati wa mchakato wa kupia kura na pengine hata baadaye. Wasiwasi huo unatokana na sababu mbali mbali zinazotajwa na wadadisi wa mambo wanaofuatilia uchaguzi huo.

Mwaka 2007 Kenya ilitumbukia katika ghasia kubwa zilizosababisha umwagikaji mkubwa wa damu ambao hauwezi kusahaulika katika historia ya taifa hilo la Afrika Mashariki. Je, matukio ya Kenya yametoa somo gani kwa wananchi wa Tanzania wanaosubiri kupiga kura?

Saumu Mwasimba amejadili suala hilo na Richard Shaba, mchambuzi wa masuala ya kisiasa na Mratibu Mipango wa wakfu wa Kijerumani wa Konrad Adenauer nchini Tanzania.