1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

TIRANA:Rais Bush afanya ziara Albania

10 Juni 2007
https://p.dw.com/p/CBt2

Rais Gorge W Bush wa Marekani amewasili nchini Albania katika ziara yake ya barani Ulaya .

Albania inatarijia kutoka kwa rais Bush kupata hakikisho la kuungwa mkono katika kujiunga na umoja wa kujihami wa nchi za Magharibi NATO pamoja na kupatikana mwafaka katika suala la hatma ya jimbo la Kosovo.Ziara ya Bush imepokelewa kwa furaha na Waalbania wengi ambao wanasema itakuwa ya manufaa kwa nchi yao na hatma jimbo la Kosovo.

Marekani inaunga mkono kwa dhati mpango wa Umoja wa mataifa wa kutaka uhuru kwa jimbo la Kosovo mwaka huu hatua ambayo inapingwa vikali na Urussi ambaye ni mshirika wa Serbia.

Ulinzi mkali umewekwa katika barabara za mji wa Tirana ambako hakutarajiwi kufanyika maandamano ya kupinga ziara hiyo.

Baadae rais Bush anatarajiwa kukamilisha ziara yake nchini Bulgaria.