1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Tume ya ukweli yaanza kazi Gambia

Sekione Kitojo
8 Januari 2019

Uchunguzi kuhusu ukiukaji wa haki za binadamu uliofanywa na utawala wa Yahya Jammeh umeanza. Tume ya ukweli katika taifa hilo imeanza kusikiliza ushahidi.

https://p.dw.com/p/3BBEi
Gambia Yahya Jammeh
Picha: picture alliance/AP Photo

Tume  ya  ukweli  katika  taifa  dogo  la  Afrika  magharibi la  Gambia  imeanza  kusikiliza  ushahidi  wakati ikianza uchunguzi kuhusu  ukiukaji  wa  haki  za  binadamu uliofanywa  na  utawala  wa  Yahya Jammeh.

Ikiwa  katika  mtindo  wa  uchunguzi  uliofanyika  nchini Afrika  Kusini  katika  enzi  ya ubaguzi  wa  rangi, tume hiyo itasikiliza ushahidi  kuhusiana  na  utawala  wa  miaka 22 wa  Jammeh uliokuwa  wa ukandamizaji  na  kuishia mwaka  2016 baada  ya  kulazimishwa  kuondoka madarakani. 

Rais Adama  Barrow ameisifu  tume  hiyo kuwa  ni  hatua kuelekea  katika  kulipknya  taifa  hilo  na  njia  ya kuwafikisha  mahakamani  wale  waliohusika  na  kufikisha mwisho madhila  ya   wahanga  na  familia.

Watetezi  wa  haki  za  binadamu  wanaushutumu  utawala kwa  kufanya  utesaji  dhidi  ya  wapinzani  na  waandishi habari, mauaji  holela, kukamatwa  na  kuwekwa  kizuwizini na  kupotea kwa  watu  katika  taifa  hilo  la  Afrika magharibi.