1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ufaransa kujiingiza kijeshi Mali: Kuona au kupotea njia?

18 Januari 2013

Hatua ya Ufaransa kujiingiza kijeshi Mali kuwazuia wanamgambo wa Kiislamu wanaolidhibiti eneo la kaskazini la nchi hiyo inazusha suala ikiwa mkoloni huyo wa zamani ameona njia ya kupita au anafanya kosa la kihisabati?

https://p.dw.com/p/17N69
A French Rafale fighter jet lands in Ndjamena, Chad, before being deployed in Mali, in this picture provided by the French Military Communications Audiovisual office (ECPAD) and taken on January 13, 2013. Al Qaeda-linked Islamist rebels in Mali launched a counter-offensive on Monday after three days of strikes by French fighter jets on their strongholds in the desert north, vowing to drag France into a long and brutal ground war. Photo taken January 13, 2013. Mandatory Credit. REUTERS/Adj. Nicolas-Nelson Richard/ECPAD/Handout (FRANCE - Tags: MILITARY POLITICS TRANSPORT) ATTENTION EDITORS - THIS IMAGE WAS PROVIDED BY A THIRD PARTY THIS PICTURE IS DISTRIBUTED EXACTLY AS RECEIVED BY REUTERS AS A SERVICE TO CLIENTS. NO SALES. NO ARCHIVES. FOR EDITORIAL USE ONLY. NOT FOR SALE FOR MARKETING OR ADVERTISING CAMPAIGNS. THIS IMAGE HAS BEEN SUPPLIED BY A THIRD PARTY. IT IS DISTRIBUTED, EXACTLY AS RECEIVED BY REUTERS, AS A SERVICE TO CLIENTS. MANDATORY CREDIT
Mali Frankreich MilitäreinsatzPicha: Reuters

Mali, koloni la zamani la Ufaransa magharibi mwa Afrika, ilikuwa ikitajwa kama mfano wa demokrasia, lakini ghafla moja mwezi Machi mwaka jana ikageuka kuwa kiini cha shaka na wasiwasi, sio tu kwa siasa za nchi hiyo, bali pia usalama wa eneo zima la kile kinachojuilikana kama Sahel, yaani eneo linalounganisha mataifa ya magharibi na kaskazini mwa Afrika.

Hiyo ni baada ya mapinduzi ya kijeshi, ambapo kundi la wanajeshi wa ngazi za kati wakiongozwa na Kapteni Amadou Sanogo walimuondoa madarakani Rais Amadou Toumane Toure, wakimlaumu kwamba alishindwa kuwapa uwezo wanajeshi kupambana na waasi wa Kituareg wa kundi la MNLA kaskazini mwa nchi hiyo.

Hadithi ikawa mbaya zaidi pale waasi hao wa Tuareg waliposhirikiana na makundi ya Kiislamu kujitangazia uhuru wa eneo lao wanaloliita Azawwad, na ikachafuka zaidi pale hata hao Watuareg nao walipozidiwa nguvu na kundi la Kiislamu la Ansar Dine, ambalo liliamua kuunda utawala wa sharia kwenye eneo hilo, ambalo linasemekana kuwa na ukubwa wa zaidi ya nchi ya Ufaransa, na likichukua zaidi ya nusu ya nchi nzima ya Mali.

Ansar Dine, kundi linalotetea imani ya Kiislamu, linaaminika kuwa na mafungamano na tawi la al-Qaida la eneo la Maghreb (AQIM) ambalo pia linashiriki mapambano hayo. Ni kutokana na matukio hayo ndipo kulipozuka wasiwasi mkubwa kimataifa juu ya kitisho cha eneo hilo kugeuzwa kuwa pepo ya magaidi.

Novemba 2012 viongozi wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Afrika Magharibi (ECOWAS) wakakubaliana kutuma kikosi cha zaidi ya wanajeshi 3,300 katika kipindi cha mwaka mzima kupambana na waasi hao, lakini hata haijafahamika hatima ya uamuzi huo, tarehe 11 Januari, Ufaransa ikapeleka rasmi wanajeshi wake nchini Mali.

Maoni Mbele ya Meza ya Duara kutoka hapa DW Bonn yanaujadili uamuzi huo wa Ufaransa. Saumu Mwasimba anaongoza mjadala akiwaalika kwa njia ya simu Salim Himid, ambaye ni mchambuzi wa siasa za Ufaransa na mkaazi Paris aliye safarini Zanzibar; Cosmas Bahali, ambaye ni mkurugenzi wa Taasisi ya Kimataifa ya Mizozo na Amani ya Kimataifa (IPCS) aliye Dar es Salaam, Tanzania; Jenerali Ulimwengu, ambaye ni mchambuzi wa masuala ya kimataifa na mwandishi wa habari Dar es Salaam pamoja na Profesa Sheikh Omar Khalfan Bizuru kutoka Rwanda.

Makala: Maoni
Mtayarishaji/Muongozaji: Saumu Mwasimba
Mhariri: Josephat Charo