1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Vyombo vya habari

Uhuru wa vyombo vya habari haujakomaa

2 Mei 2017

Kila mwaka, tarehe 3 Machi, dunia inaadhimisha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari. DW inaangalia hatua zilizopigwa na changamoto zilizopo katika sekta ya habari barani Afrika kama vile wanasiasa kuingilia sekta hiyo.

https://p.dw.com/p/2cDRE
Tanzania We need freedom of press
Picha: DW/A. Juma

FE:Kinagaubaga 02/03/05.05 (Freedom of the Media Tanzania) - MP3-Stereo

Huku dunia ikiadhimisha siku ya uhuru wa habari , waandishi habari nchini Uganda wanazidi kukabiliwa na mazingira magumu ya kazi kutokana na sheria kandamizi zinazobuniwa kila kukicha. Aidha makabiliano na vyombo vya usalama hasa polisi na vitisho vya mara kwa mara kutoka kwa wanasiasa na hata waajiri wao vimeshudiwa mara kwa mara. Haya ni licha ya madai ya utawala nchini humo kwamba unalinda kwa dhati uhuru wa habari.