Umeshawahi kuziona mboga hizi? Kama bado, basi nikujulishe tu kuwa zinaitwa ''Asparagus'' nyeupe. Msimu wa kilimo cha mboga aina ya Asparagus nyeupe umeanza nchini Ujerumani. Kwa kawaida msimu huo unaanza katikati ya mwezi Aprili hadi Juni 24. Mboga hizo zinauzwa sana kwenye maduka makubwa, huku bei ikielezwa kutofautiana kutokana na urefu na ncha ya mboga hiyo. Kurunzi Ujerumani 25.04.2019