1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani yagombea ubingwa wa mpira wa mkono

2 Februari 2007
https://p.dw.com/p/CCVz

Na sasa kwenye uwanja wa spot:

Mwenyeji Ujerumani imefanikiwa kuingia fainali katika mashindano ya ubingwa wa mpira wa mkono. Ujerumani imewafunga mabingwa wa Ulaya,Ufaransa mabao 32-31 mjini Cologne,katika nusu fainali baada ya mchezo kurefushwa mara mbili.Ujerumani iliyowahi kuwa mabingwa mwaka 1938 na 1978,sasa inatazamia kujinykulia ubingwa kwa mara ya tatu, itakapokumbana na Poland katika fainali siku ya Jumapili.Na mjini Hamburg,Poland pia imeifunga Denmark mabao 36-33 baada ya mchezo huo vile vile kurefushwa mara mbili.