1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani yailaza Uingereza bao nne kwa moja.

Halima Nyanza28 Juni 2010

Mashindano ya kombe la dunia ya soka yanaendelea leo nchini Afrika kusini, baada ya timu mbili za Ujerumani na Argentina jana kufanikiwa kuingia robo fainali za mashindano hayo.

https://p.dw.com/p/O4gm
Vikosi vya Ujerumani na Uingereza vilivyopambana jana.Picha: AP/Montage DW

Mashindano ya kombe la dunia ya soka yanaendelea leo nchini Afrika kusini, baada ya timu mbili za Ujerumani na Argentina jana kufanikiwa kuingia robo fainali za mashindano hayo.

Ujerumani ilifanikiwa kusonga mbele baada ya kuibamiza Uingereza mabao manne kwa moja, ambapo magoli yake yalifungwa na Miroslav Klose na Lukas Podolski katika kipindi cha kwanza na mengine mawili yalifungwa na Thomas Mueller katika kipindi cha pili.

Deutsche Fußballfans in Berlin WM 2010 Flash-Galerie
Washabiki wa timu ya taifa ya soka ya Ujerumani, wakishangilia timu yao, ilipoinyuka Uingereza goli nne kwa moja, hapo jana, nchini Afrika kusini.Picha: AP

Goli la Uingereza la kufutia machozi lilifungwa na Matthew Upson.

Na katika mchezo mwingine uliochezwa hapo jana, Argentina nayo iliweza kusonga mbele kwa kuifunga Mexico, mabao matatu kwa moja.

Argentina itapambana na Ujerumani katika robo fainali, Jumamosi ijayo.