1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Afrika wachanga fedha kusaidia wahanga wa ukame

Martin,Prema/zpr26 Agosti 2011

Mkutano wa Umoja wa Afrika wa kuchangia fedha za kuwasaidia wahanga wa janga la njaa katika Pembe ya Afrika, umemalizika Addis Ababa nchini Ethiopia, kwa kuahidi msaada wa dola milioni 352.

https://p.dw.com/p/Ri7Z
Kenya: drought leaves dead and dying animals in northen Kenya Dead and dying animals at the Dambas, Arbajahan, Kenya, which has dried up due to successive years of very little rain. Africa's climates have always been erratic but there is evidence that global warming is increasing droughts, floods and climate uncertainty and unpredictability. Picture credit: Brendan Cox / Oxfam Picture date: 15 January 06 +++CC / Brendan Cox / Oxfam+++ am 10.1.2004 aufgenommen am 23.11.2010 ins CMS gestellt Lizenz: http://creativecommons.org/licenses/by-nc-nd/2.0/deed.de
Ukame umeteketeza mifugo na mavunoPicha: CC / Brendan Cox / Oxfam

Mkutano huo wa kilele umehudhuriwa na viongozi wanne tu wa taifa na serikali, ikiwa ni wachache kuliko ilivyotarajiwa. Benki ya Maendeleo ya Afrika imeahidi msaada wa dola mlioni 300. Mkurugenzi wa shirika la misaada la Oxfam barani Afrika, Irungu Houghton amesikitika kuwa serikali za Afrika hazukushughulikia vya kutosha tatizo hilo.

Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, bado kunahitajiwa dola bilioni 1.1 ili kuweza kuzuia madhara makubwa zaidi kutokana na ukame mbaya kabisa kushuhudiwa tangu miongo kadhaa katika Pembe ya Afrika. Zaidi ya watu milioni 12 wanakabiliwa na njaa nchini Somalia, Ethiopia, Eritrea, Djibouti, Kenya na Uganda.