1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Mataifa wailaumu DRC kubana uhuru wa maoni

Saumu Mwasimba
2 Desemba 2016

Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya uhuru wa kutoa maoni ameishutumu serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwa kukiuka sheria ya kimataifa juu ya haki za binadamu.

https://p.dw.com/p/2Td3y
Demokratische Republik Kongo Joseph Kabila
Picha: Getty Images/AFP/J.D. Kannah

Msimamo huu unakuja huku serikali ya Rais Joseph Kabila ikichukuwa hatua yake ya kuyazima matangazo ya radio pamoja na kuwakamata waandishi habari nchini humo.

Mtaalamu huyo, David Kaye, anasema sheria iliyopitishwa Novemba 12 ya kuyazuia mashirika ya habari ya kimataifa kuendesha kazi zao nchini Kongo hadi pale yatakaposaini makubaliano na vyombo vya habari vya ndani au kuanzisha matawi yao yatakayosimamiwa na Wakongomani ni uvunjaji wa sheria za kimataifa.

Mtaalamu huyo wa Umoja wa Mataifa amesema kupitia taarifa yake kwamba kuzimwa kwa sauti za kuikosoa serikali kwa kupitia njia ya kuwakamata, kuwadhibiti na kupitia njia nyingine za zinazotumiwa na serikali kudhibiti ni mambo yanayotishia usalama wa nchi hiyo.