1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Viongozi wa Ulaya na Afrika walaumiwa na waandishi mashuhuri

4 Desemba 2007
https://p.dw.com/p/CX4U

Kundi la waandishi maarufu limewatuhumu viongozi wa Ulaya na Afrika kwa kuwa na uoga wa kisiasa kwa kutoyapa kipaumbe masuala ya Darfur na Zimbabwe katika ajenda ya mkutano wa kilele wa Umoja wa Ulaya na Afrika utakaofanywa Lisbon nchini Ureno.

Waandishi hao,ikiwa ni pamoja na Vaclav Havel,Ben Okri na washindi wa Tuzo ya Nobel Gunter Grass na Nadine Gordimer,wamewashutumu wanasiasa hao kuwa wanayapa kisogo mizozo mibaya kabisa ya kiutu duniani.Wamesema,Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe anawakandamiza wapinzani wake na anateketeza uchumi wa nchi hiyo.Viongozi hao vile vile wanalaumiwa kuwa suala la Darfur halikuwekwa katika ajenda ya mkutano wao mjini Lisbon.