1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Waandamanaji wataka adhabu kali zaidi

30 Novemba 2007
https://p.dw.com/p/CVGT

Mamia ya watu wameandamana katika mji mkuu wa Sudan,Khartoum wakilaani adhabu iliyotolewa kwa mwalimu wa Kingereza.Mwalimu Gillian Gibbons ameadhibiwa kifungo cha siku 15 baada ya kufikishwa mahakamani kwa mashtaka kuwa aliitusi dini ya Kiislamu alipowaruhusu wanafunzi wake kutoa jina la Mohamed kwa dubu la sanamu yaani „teddy bear“.Waandamanaji wamesema,mwalimu huyo apewe adhabu ya kifo.