1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Waasi wa ADF waushambulia mji wa Beni

Amina Mjahid
23 Julai 2019

Waasi kutoka Uganda wa kundi la ADF wamewaua raia zaidi ya 20 mjini. Mauwaji yaliyotokea baada ya rais Félix Tshisekedi kuahidi kuwatokomeza waasi hao, yamewakera viongozi wa mashirika ya kiraia katika eneo hilo.

https://p.dw.com/p/3Maoq
DR Kongo Alltagsleben in Beni in der nähe von dem Kreisverkehr Nyamwissi
Picha: DW/W. Bashi

Kubwa katika yote ni mauwaji ya watu kumi yaliyofanywa na ADF usiku wa kuamkia leo katika kata ya Mabasele, katika mji mdogo wa Oicha, ambako watu kumi wameuawa kwa kukatwa kwa mapanga.

Akizungumza na idhaa ya kiswahili ya DW, mwenyekiti wa mashirika ya kiraia katika mji wa Beni Kizito Bin Hangi alisema, kuwa haelewi hali ya kusuasua kwa operesheni za kijeshi dhidi ya waasi kutoka Uganda ADF katika eneo hili.

Akizungumzia maeneo yaliyoshuhudia mauwaji hayo, Kizito Bin Hangi anamuomba rais Félix Tshisekedi kutekeleza ahadi yake kwa raia wa Beni, wakati wa ziara yake katika eneo hilo.

Soldaten der FARDC in der Nähe von Beni Kongo im Einsatz gegen Islamisten aus UgandaJanuar 2014
Picha: Getty Images/AFP/Alain Wandimoyi

Mauwaji ya usiku wa leo yakiwa yanatokea baada ya yale yaliyofanywa na waasi hao katika vitongoji vya Eringeti, Mayimoya, Mangboko na Malolu, yamezusha hofu mioyoni mwa wakaazi, waliokuwa na matumaini kwamba amani ya kudumu itarejea katika eneo hili. 

Hatua itakayowapelekea kurudi katika mashamba waliyoyahama wakihofia maisha, na kuanzisha upya shughuli za kilimo.

Jeshi la serikali ya DRC yafanikiwa kuwaangamiza baadhi ya waasi

Katika kuwashambulia waasi wa ADF, baada ya kuwauwa raia, majeshi ya serikali yalifanikiwa kuwauwa waasi wanne, na kuchukuwa silaha mbili kutoka waasi hao.

"Hongera kwa majeshi ya serikali ya Kongo, kwa kazi walioifanya ya kuwauwa waasi wanne na kuchukuwa silaha zao,"alisema Meya wa Beni Bwanakawa Masumbuko Nyonyi.

Idadi ya waasi wa ADF waliouawa katika operesheni za kijeshi, imeongezeka na kufikia watano,kama anavyotueleza Sheikh Djamali Mussa,mwenyekiti wa mashirika ya kiraia katika kongamano la Batangi Mbau

Mauwaji ambayo kwa sasa yanakita mizizi, yamewapelekea wadadisi wa maswala ya usalama,kuiomba serikali ya DRC kuomba msaada wa kijeshi toka nchi jirani ya Uganda, ADF wakiwa ni maadui wa nchi zote mbili.

Ombi hilo haijulikani ikiwa litakubaliwa na serikali zote mbili yaani Kongo na Uganda.