1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wahanga wa janga la njaa wahitaji msaada zaidi

Martin,Prema/ap,rtr25 Septemba 2011

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon ametoa mwito kwa Umoja wa Mataifa kutoa mchango zaidi wa fedha kuwasaidia wahanga wa janga la njaa katika Afrika ya Mashariki.

https://p.dw.com/p/Rnd8
NEW YORK, Aug. 27, 2011 UN Secretary-General Ban Ki-moon speaks to media during a press conference at the headquarters in New York, the United States, Aug.26, 2011. After a meeting with heads of regional organizations on Friday afternoon, Ban told reporters that the international community, including the UN, stands prepared to provide support to Libya in the aftermath of its violent, months-long conflict
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moonPicha: picture alliance ZUMA Press

Katibu Mkuu Ban, alipozungumza mjini New York, alisema, katika kipindi cha mwaka mmoja pekee, kunahitajiwa msaada mwingine wa dola milioni 700 ili kuweza kuokoa maisha ya watu milioni 13 walioathirika nchini Somalia, Kenya na Ethiopia.

Wakati huo huo, Benki ya Dunia imearifu kuwa itaongeza msaada wake hadi kufikia takriban dola bilioni 1 nukta 9.