1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Waislamu nchini Kenya Waandamana dhidi ya kukamatwa kwa Mhubiri wa Kijamaica

15 Januari 2010

Nchini Kenya Waislamu leo hii wameandamana dhidi ya kukamatwa kwa Mhubiri wa Jamaica Sheikh Abdullah Al Faisal.

https://p.dw.com/p/LWvQ
Jiji la Nairobi kulikofanyika maandamano kupinga kukamatwa kwa sheikh Al FaisalPicha: picture-alliance/dpa

Mzozo kuhusu kukamatwa kwa mhubiri raia wa kutoka Jamaica, Sheikh Abdulla Al Faisal, umechukuwa sura mpya baada ya jamii ya Waislamu nchini humo kuandamana leo kuishinikiza serikali kumuachilia huru mara moja Mhubiri huyo, anayetuhumiwa kuwa mfuasi wa kundi la kigaidi la Al Qaeda.

Katika mji mkuu wa Nairobi, Polisi walilazimika kutumia mabomu ya kutoa machozi kuwatimua wandamanaji hao na watu watano wadaiwa kufa.

Katika mji wa Mombasa kama anavyoarifu mwandishi wetu Eric Ponda pia kulifanyika maandamano hayo.

Mwandishi:Eric Ponda

Mhariri:Aboubakary Liongo