1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wanaharakati wazungumzia kukamatwa kwa wakeketaji haramu

Mjahida18 Desemba 2013

Kufuatia kuwakamata wanawake 38 nchini Tanzania,kwa kuwafanyia ukeketaji haramu kundi la wasichana wa mji wa Same, wanaharakati wamelipokea suala hilo kwa mtazamo tofauti, wakitaka sheria ifanye kazi.

https://p.dw.com/p/1AbqA
Wanawake wakibeba mabango ya kusisitiza kusimamishwa kwa ukeketaji
Picha: picture-alliance/dpa

Wanawake hao walikamatwa wakati wakicheza ngoma za asili katika nyumba moja, ambako polisi iliwakuta wasichana 21 wenye umri kuanzia miaka mitatu hadi 15, waliokwisha keketwa. Flora Nzema amezungumza na Jovita Mlay mwanaharakati wa masuala ya ukeketaji, ambaye kwanza anaelezea namna alivyoipokea hatua ya kuwafikisha wahusika mahakamani. Je kufikishwa mahakamani kwa wanaoounga mkono vitendo vya ukeketaji kutasaidia kukomesha vitendo hivyo nchini Tanzania?

Mwandishi: Flora Nzema

Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman