1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Washauri wa rais Obama wakutana kuijadili Syria

24 Agosti 2013

Washauri wa rais Barack Obama watakutana katika ikulu ya Marekani ya White House mwishoni mwa wiki hii kujadili nafasi mbali mbali za nchi hiyo, ikiwa ni pamoja na hatua za kijeshi, dhidi ya serikali ya Syria.

https://p.dw.com/p/19VVc
People, affected by what activists say is nerve gas, are treated at a hospital in the Duma neighbourhood of Damascus August 21, 2013. Syrian activists accused President Bashar al-Assad's forces of launching a nerve gas attack on rebel-held districts near Damascus on Wednesday that they said killed more than 200 people. There was no immediate comment from Syrian authorities, who have denied using chemical weapons during the country's two-year conflict, and have accused rebels of using them, which the rebels deny. REUTERS/Bassam Khabieh (SYRIA - Tags: POLITICS CIVIL UNREST CONFLICT)
Wahanga wa gesi ya sumu nchini Syria wakipatiwa matibabuPicha: Reuters

Washauri wa rais Barack Obama watakutana katika ikulu ya Marekani ya White House mwishoni mwa wiki hii kujadili nafasi mbali mbali za nchi hiyo , ikiwa ni pamoja na hatua za kijeshi , dhidi ya serikali ya Syria.

Mjadala huo utahusu iwapo serikali ya Syria ilitumia silaha za kemikali katika shambulio mapema wiki hii.

U.S. President Barack Obama makes a statement about the violence in Egypt while at his rental vacation home on the Massachusetts island of Martha's Vineyard in Chilmark August 15, 2013. REUTERS/Larry Downing (UNITED STATES - Tags: POLITICS)
Rais Barack ObamaPicha: Reuters

Maafisa wa Marekani wamesema jana Ijumaa(23.08.2013) kwamba iwapo rais Obama atashiriki katika mkutano huo , hali inayoonekana kuwa kuna uwezekano , itakuwa kikao chake cha kwanza kamili akiwa na wasaidizi wake wa ngazi ya juu wa sera za mambo ya kigeni tangu shambulio la gesi ya sumu siku ya Jumatano katika kitongoji kimoja mjini Damascus.

Uamuzi bado

Lakini afisa huyo ambaye amezungumza kwa masharti ya kutotajwa jina, ametahadharisha dhidi ya matarajio kuwa uamuzi wowote wa mwisho huenda unaweza kutolewa katika duru hii ijayo ya majadiliano.

Wakati huo huo wizara ya ulinzi inayaweka tayari majeshi yake iwapo rais Barack Obama ataamua kuchukua hatua ya kijeshi dhidi ya Syria, amesema waziri wa ulinzi wa Marekani Chuck Hagel siku ya Ijumaa.

WASHINGTON, DC - APRIL 17: Defense Secretary Chuck Hagel testifies during a Senate Armed Services Committee hearing on Capitol Hill, April 17, 2013 in Washington, DC. The committee is hearing testimony from Secretary Hagel on the Defense Departments budget request for FY2014 and beyond. (Photo by Mark Wilson/Getty Images)
Waziri wa ulinzi wa Marekani Chuck HagelPicha: Getty Images

Huku kukiwa na miito kadha ya kujingilia kati kijeshi baada ya utawala wa Syria kutumia kile kinachodaiwa kuwa ni silaha za kemikali wiki hii, makamanda wa jeshi la Marekani wamenajitayarisha kwa uwezekano mbali mbali kwa rais Obama iwapo ataamua kuanzisha mashambulio dhidi ya utawala wa Syria, Hagel amewaambia waandishi habari akiwa katika ndege yake iliyokuwa ikielekea nchini Malaysia.

Lakini amekataa kutoa taarifa zaidi kuhusiana na wapi majeshi ya Marekani yatawekwa pamoja na vifaa huku kukiwa na hali ya kuongezeka kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Syria.

"Wizara ya ulinzi inawajibu wa kumpa rais uwezekano kwa kila aina ya hali," Amesema Hagel.

epa03363568 USS Blue Ridge, the command ship of the U.S. 7th Fleet, enters a naval base in South Korea's largest port city of Busan amid a welcome by the South Korean Navy, 17 August 2012. The ship arrived in South Korea to join the Ulchi Freedom Guardian (UFG), an annual military exercise between the two nations, set for 20-31 August 2012. EPA/STRINGER SOUTH KOREA OUT +++(c) dpa - Bildfunk+++
Manowari ya jeshi la MarekaniPicha: picture alliance / dpa

Meli zawekwa katika tahadhari

Amesema wakati afisa wa wizara ya ulinzi akisema kuwa jeshi la majini litapanua uwapo wake katika bahari ya Mediterranean kwa kuweka meli ya nne ikiwa na uwezo wa kubeba makombora.

Kikosi cha sita cha jeshi la Marekani , kikiwa na wajibika katika bahari ya Mediterranean , kimeamua kuibakisha manowari ya USS Mahan katika eneo hilo badala ya kuiruhusu kurejea nyumbani katika bandari ya Norfolk , jimboni Virginia.

Manowari nyingine tatu hivi sasa zimewekwa katika eneo hilo, USS Gravely , USS Barry na USS Ramage. Meli zote nne za kivita zina makombora kadha ya Tomahawk.

Meli hizo za ziada zinairuhusu wizara ya ulinzi kuchukua hatua za haraka iwapo Obama ataamuru shambulio la kijeshi.

"Rais ameitaka wizara ya ulinzi kutoa mapendekezo mbali mbali. Pamoja na hayo , wizara ya ulinzi iko tayari na imekuwa tayari kutoa uwezekano wa aina yoyote kwa rais wa Marekani ," Hagel amesema.

FILE -This undated photo provided by Northrop Grumman Corp., shows a pre-production model of the F-35 Joint Strike Fighter. The Pentagon on Friday grounded its fleet of F-35 fighter jets after discovering a cracked engine blade in one plane. The problem was discovered during what the Pentagon called a routine inspection at Edwards Air Force Base, California, of an F-35A, the Air Force version of the sleek new plane. The Navy and the Marine Corps are buying other versions of the F-35, which is intended to replace older fighters like the Air Force F-16 and the Navy F/A-18. All versions , a total of 51 planes , were grounded Friday, Feb. 22, 2013 pending a more in-depth evaluation of the problem discovered at Edwards. None of the planes have been fielded for combat operations; all are undergoing testing.AP Photo/Northrop Grumman, File) no sales
Ndege ya kivita ya jeshi la marekani F-35Picha: picture-alliance/ap

Mkuu hiyo wa wizara ya ulinzi pamoja na maafisa wengine wa wizara ya ulinzi katika utawala wa rais Obama wameweka wazi kuwa hakuna uamuzi ulikwisha chukuliwa iwapo kuchukua hatua za kijeshi dhidi ya utawala wa rais Bashar al-Assad.

Magazeti ya Marekani yamekuwa yakieleza kuwa kuna hali ya kutokubaliana ndani ya utawala wa Marekani kuhusiana na hatari ya kujiingiza katika vita vingine katika mashariki ya kati.

Mwandishi : Sekione Kitojo / afpe / rtre

Mhariri : Sudi Mnette