WASHINGTON: Bush atetea sera za vita vya Irak
15 Julai 2007Matangazo
Rais George W.Bush wa Marekani kwa mara nyingine tena amejitetea dhidi ya wakosoaji wa sera za serikali yake nchini Irak.Bush amekiri kuwa ripoti iliyotolewa juma hili imesema kuwa serikali ya Irak imeshindwa kutekeleza mageuzi muhimu kuhusu masuala manane mbali mbali,lakini vile vile imeridhisha katika mambo manane mengine.Kwa hivyo amesema,kuna sababu ya kuwa na matumaini.
Bush akaeleza kwamba msingi wa mkakati ni kuwa maendeleo ya usalama yatafungua njia ya kuleta maendeleo ya kisiasa.Ripoti yaonyesha kuwa masharti yaweza kubadilika,maendeleo yanaweza kupatikana na vita vya Iraq lazima vipate ushindi.