1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 21 wahukumiwa kifo Misri

Mohamed Dahman26 Januari 2013

Watu 22 wameuwawa (26.01.2013) katika mapambano ya kupinga kuhukumiwa kwa adhabu ya kifo kwa watu 21 kutokana na kuhusika kwao katika ghasia za soka zilizosababisha vifo vya watu 74 wakati wa mechi ya soka mwaka jana

https://p.dw.com/p/17S7A
Egyptian fans of Al-Ahly football club celebrate outside the club's headquarters in Cairo on January 26, 2013 after a court sentenced 21 people to death over a football riot that killed more than 70 people last year. The clashes in Port Said in February last year between fans of home side Al-Masry and Cairo's Al-Ahly had left more than 70 people dead and sparked days of violent protests in Cairo, in which another 16 people were killed. AFP PHOTO / MOHAMMED ABED (Photo credit should read MOHAMMED ABED/AFP/Getty Images)
Washabiki wa SokaPicha: Mohammed Abed/AFP/Getty Images

Watu sabini na tatu wakiwemo maafisa wa michezo na polisi wanashtakiwa kwa madai ya mauaji ya kudhamiria au uzembe kuhusiana na ghasia hizo zilizotokea kwenye uwanja wa Port Said hapo mwezi wa Februari.

Ghasia hizo zilizuka kati ya mashabiki hasimu wa timu wenyeji wa pambano hilo Al Masry na Al-Ahly wakati wa michuano ya ligi kuu na kusababisha watu 74 kupoteza maisha yao.Hayo yalikuwa ni maafa makubwa kuhusiana na mchezo wa mpira wa miguu kuwahi kushuhudiwa nchini humo katika kipindi cha zaidi ya muongo mmoja.

Polisi wawili ni miongoni mwa watu waliouwawa katika ghasia za Jumamosi na kwa mujibu wa mkurugenzi wa afya katika mji wa Port Said watu zaidi ya 200 wamejeruhiwa.

Washitakiwa wengine kuhukumiwa Machi

Hakimu wa mahakama amesema hukumu kwa washtakiwa wengine 52 waliobakia itatolewa tarehe tisa mwezi wa Machi. Kutokana na sababu za usalama takriban washtakiwa wote hawakuwako mahakamani mjini Cairo wakati hukumu hiyo ilipotolewa.

Washtakiwa wote wana haki ya kukata rufaa na kati ya wale waliohukumiwa Jumamosi hakuna askari yoyote.

Mahakama ya Cairo iliotowa hukumu hiyo sasa imeikabishi kwa kiongozi wa juu wa dini nchini humo kwa maoni ya mwisho.Utekelezaji wa hukumu za adhabu za kifo nchini Misri lazima uidinishwe na Mufti Mkuu.

Katika mji wa Port Said kumezuka mapambano kati ya waandamanaji na polisi. Mashabiki wa timu ya Al-Masry na familia za washtakiwa wanasema kulikuwa na mkono wa kisiasa katika kesi hiyo.

Polisi ilitumia gesi ya kutowa machozi kutawanya waandamanaji ambao walijaribu kulivamia gereza wanakoshikiliwa washtakiwa.

Timu ya Al-Ahly yasherehekea hukumu

Hata hivyo mamia ya mashabiki wa timu ya Al-Ahly walisherehekea hukumu hiyo kwa kuwasha fataki na kuimba nyimbo katika mitaa ya Cairo. Kulikuweko na nderemo ndani na nje ya mahakama katika mji mkuu huo wakati hukumu hiyo ikisomwa mahakamani.Wanawake walipiga vigeregere,familia na jamaa za wahanga walikumbatina na kupiga mayowe ya "Allahu Akbar".

Al Ahly fans, also known as "Ultras", celebrate and shout slogans in front of the Al Ahly club after hearing the final verdict of the 2012 Port Said massacre in Cairo January 26, 2013. Twenty-two people were killed on Saturday in violence that erupted in Port Said, northeast of Egypt's capital, after protesters took to the street angry that people from their city had be blamed for a soccer disaster, state television said. REUTERS/Amr Abdallah Dalsh (EGYPT - Tags: POLITICS CIVIL UNREST SPORT SOCCER TPX IMAGES OF THE DAY CRIME LAW)
Washabiki wa Al Ahly wakishangiliaPicha: Reuters

Mapambano ya Port Said yamepelekea kuwekwa kwa wanajeshi katika mji huo kulinda taasisi muhimu za serikali na kurudisha usalama.

Vituo viwili vya polisi vilivamiwa na milio mizito ya risasi ilikuwa inasikikika kutoka kitongoji cha Al Manakh.Magari ya kubebea wagonjwa yamekuwa yakipeleka majeruhi hospitali na maduka na shughuli zote za biashara zilifungwa wakati waandamanaji wakiunguza mipira barabarani.Misikiti katika mji huo imekuwa ikitowa wito kwa watu kujitolea damu.

Uamuzi huo umekuja masaa machache baada ya vikosi kuwekwa katika mji wa karibu wa mwambao wa Suez kufuatia mapambano kati ya polisi na waandamanaji wanaopinga serikali kusababisha vifo vya watu tisa.

Ultras soccer fans gather around tyres they burnt over a bridge during a rally to demand justice for 74 people killed in a stadium stampede last year, in central Cairo January 23, 2013. A court is expected to rule on Saturday in the case brought against 61 people charged with murder and 12 others, including nine police officers and three al-Masry club officials, with helping cause the disaster at Port Said stadium during a match between Cairo's Al Ahly and local side al-Masry. REUTERS/Stringer (EGYPT - Tags: CIVIL UNREST SPORT SOCCER)
Wanadamanaji wanaopinga uamuziPicha: Reuters

Mapambano ya Suez ni mabaya kabisa katika wimbi la ghasia lililozuka nchini kote Misri hapo Ijumaa wakati wa maadhimisho ya miaka miwili ya vuguvgu lilimn'gowa madarakani rais wa zamani Hosni Mubarak.

Muungano wa Ukombozi wa Taifa ambao ni muungano mkuu wa upinzani wa vyama na makundi ya vuguvugu wenye kupinga utawala wa Waislamu wa itikadi kali nchini humo umetowa wito miongoni mwa mambo mengine kuundwa kwa serikali ya ukombozi wa taifa venginevyo hautoshiriki katika uchaguzi ujao wa bunge.

Rais Mohamed Mursi ametowa wito wa kuwepo kwa utulivu na kuahidi kwamba serikali itawafikisha mbele ya sheria wale wenye kuvunja sheria za nchi hiyo. Ametaka watu waheshimu misingi ya mapinduzi ya Misri na kutowa maoni yao kwa uhuru na kwa amani.

Mwandishi : Mohamed Dahman/afp/dpa
Mhariri: Sudi Mnette