1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Waumini wafyatuliwa risasi nchini Marekani

10 Desemba 2007
https://p.dw.com/p/CZW9

Watu 5 wameuawa baada ya kupigwa risasi katika makanisa mawili kwenye jimbo la Colorado nchini Marekani.Katika shambulizi la kwanza watu 4 walipigwa risasi nje ya kanisa kubwa la Kiinjili mjini Colorado Springs.Hapo awali,watu 2 waliuawa na 2 wengine walijeruhiwa,ukingoni mwa mji wa Denver.Katika shambulizi hilo mtu mwenye bunduki aliingia katika kituo cha kuwafunza wamisionari vijana.Polisi hawajui ikiwa kuna uhusiano kati ya mashambulizi hayo mawili.