1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Waziri wa Ulinzi wa Marekani Mattis ziarani china

Sekione Kitojo
27 Juni 2018

Waziri wa ulinzi wa Marekani Mattis na viongozi wa China wameonesha hali ya maelewano leo, wakizungumzia kuhusu ushirikiano zaidi  wa kijeshi na majadiliano ya wazi baina ya nchi hizo. 

https://p.dw.com/p/30PGo
US-Verteidigungsminister Mattis in China
Picha: AFP/Getty Images/M. Schiefelbein

Pamoja  na  maelewano  hayo  ya  mazungumzo  zaidi  baina  yao  lakini  kuna hali  pia  ya  wasi  wasi  inayotokota pamoja  na  vita vya  kibishara vinavyoelekea kukaribia.

US-Verteidigungsminister Jim Mattis
Waziri wa ulinzi wa Marekani Jim Mattis Picha: picture-alliance/dpa/AP PhotoT. V. Minh

Katika  matamshi  ya  mwanzo  kabla  ya  mkutano  wa Mattis  na  rais  wa  China  Xi Jinping  pamoja  na  waziri wa  ulinzi  wa  China Wei Fenghe, viongozi hao  waliepuka kutaja  chochote  juu  ya  mada  ambazo  hapo  kabla zilikuwa mbele  katika  uhusiano  wao  na  kutafuta sehemu muhimu  ya  mazungumzo  yao,  masuala  kama Taiwan,  China  kulifanya eneo  la  bahari ya  kusini  ya China  kuwa  la  kijeshi pamoja  na  majadiliano yanayoendelea  na  Korea  kaskazini  kufikisha  mwisho mpango  wake  wa  kinyuklia.

Badala  yake , walilenga  katika  umuhimu  wa  uhusiano wa  kijeshi  kati  ya  China  na  Marekani na  vipi kuuendelea  uhusiano  huo. Waziri wa  ulinzi  wa  Marekani Jim Mattis  alisema.

China  Boao-Forum
Rais wa China Xi JinpingPicha: picture-alliance/Xinhua/Li Xueren

"Nitarudia  matamshi  yako katika  suala  hili  juu  ya umuhimu  unaowekwa  katika  ziara  kati  ya  mataifa  haya mawili, kuhusu ushirikiano  wa  kijeshi. Ndio sababu  niko hapa, kujadili  mfumo  wa  mkakati  ambao kwa  pamoja tunafanyakazi. Na  nafikiri  ni  muhimu  mno kwamba tuna majadiliano  kama  haya  ya  wazi, kwa  kuangalia  mbele katika  njia  ambayo  tunaweza  kushirikiana  kila inapowezekana  na  kujadili tofauti  zetu kama tunavyoweza baina ya  mataifa  yetu  makubwa mawili."

Nia thabiti ya  ulinzi wa mipaka  na utaifa

Maelezo  kuhusu mkutano  wa  Mattis  asubuhi  pamoja  na waziri  wa  ulinzi Wei , yaliyotolewa  na  gazeti  la  kila  siku la  China , ilisema  waziri  wa  ulinzi wa  China  aliweka msimamo  wa  China  na  wasi  wasi  wake  kuhusu Taiwan, bahari ya  kusini  mwa  China na  Korea  kaskazini, lakini  halikutoa taarifa  zaidi.

Wei  alisisitiza  kutokuwa  na mzozo, bila mapambano, kuheshimiana  na  ushirika  wa faida  kwa  pande zote  pamoja  na dhamira thabiti  ya kijeshi  katika  ulinzi  wa  mipaka  yake, usalama  na maendeleo ya  kimaslahi. Waziri  wa  ulinzi  wa  China Wei Fenghe alisema.

"Mheshimiwa  waziri wa ulinzi , nafahamu  kwamba  ulikuwa mwanajeshi  kwa  miaka  mingi na  maneno  yako yanabeba  uzito  wa  kisiasa  na  katika  duru  za  kijeshi."

US-Verteidigungsminister Mattis in China
Waziri wa ulinzi wa Marekani Jim Mattis akipokelewa na mwenyeji wake Wei Fenghe(kulia)Picha: AFP/Getty Images/M. Schiefelbein

Ziara  ya  Mattis pia  inakuja  huku  kukiwa  na  vita  vya kibiashara  vikitokota  baina  ya  mataifa  hayo  makubwa duniani  kiuchumi.  Rais Donald Trump  tayari  ameweka ushuru  wa  asilimia  25 kwa chuma  cha  pua  kutoka China na asilimia  10  katika madini  ya  bati.

Mwandishi: Sekione  Kitojo / ape

Mhariri: Yusuf Saumu