1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wimbledon: Lisicki asalim amri kwa Bartoli

7 Julai 2013

Bingwa wa mchezo wa tennis kwa wanawake katika mashindano ya Wimbledon Marion Bartoli amesisitiza kuwa namna alivyocheza siku ya Jumamosi(06.07.2013) huenda ni mwanzo wa ukurasa wa mafanikio yake katika mchezo huo.

https://p.dw.com/p/193JC
Marion Bartoli of France holds her trophy, the Venus Rosewater Dish, after defeating Sabine Lisicki of Germany in their women's singles final tennis match at the Wimbledon Tennis Championships, in London July 6, 2013. REUTERS/Stefan Wermuth (BRITAIN - Tags: SPORT TENNIS TPX IMAGES OF THE DAY)
Marion Bartoli bingwa wa WimbledonPicha: REUTERS/Stefan Wermuth

Bartoli alipata ushindi wake wa kwanza wa Grand Slam siku ya Jumamosi wakati Mfaransa huyo alipofanikiwa kumshinda Sabine Lisicki kutoka Ujerumani kwa seti 2-0 , 6-1 na 6-4 katika fainali ya Wimbledon.

Marion Bartoli of France (R) embraces Sabine Lisicki of Germany after defeating her in their women's singles final tennis match at the Wimbledon Tennis Championships, in London July 6, 2013. REUTERS/Toby Melville (BRITAIN - Tags: SPORT TENNIS)
Wimbledon-Finale in London Sabine Lisicki Marion BartoliPicha: REUTERS/Toby Melville

Bartoli mwenye umri wa miaka 28, ambaye alishindwa na Venus Williams katika fainali iliyopita ya Grand Slam ya Wimbledon mwaka 2007 , ni mwanamke wa tano mwenye umri mkubwa kiasi kuwa mshindi kwa mara ya kwanza wa mashindano makubwa.

Sabine Lisicki of Germany reacts during her women's singles final tennis match against Marion Bartoli of France at the Wimbledon Tennis Championships, in London July 6, 2013. REUTERS/Stefan Wermuth (BRITAIN - Tags: SPORT TENNIS)
Wimbledon-Finale in London Sabine LisickiPicha: REUTERS/Stefan Wermuth

Aendelea kutabasamu

Kwa upande wake Sabine Lisicki kama kawaida yake alikuwa akitabasamu huku akikiri kuwa alikuwa na wasi wasi mwingi kabla na wakati wa mchezo na kupoteza mchezo huo muhimu kwake na kwa Ujerumani kwa jumla.

Mjerumani huyo alionekana wazi kuwa fainali yake ya kwanza ya Wimbledon ilikuwa ngumu na alionekana dhahiri kuwa alikuwa anaelekea kupata kipigo cha kudhalilisha cha huenda 6-1 na 6-1. Lakini aliweza kupata ushindi katika michezo mitano mfululizo na kurejesha hali ya heshima .

Marion Bartoli of France (L) holds her trophy, the Venus Rosewater Dish, after defeating Sabine Lisicki of Germany (R) in their women's singles final tennis match at the Wimbledon Tennis Championships, in London July 6, 2013. REUTERS/Toby Melville (BRITAIN - Tags: SPORT TENNIS)
Wimbledon-Finale in London Marion Bartoli Sabine LisickiPicha: REUTERS/Toby Melville

Alibubujikwa na machozi uwanjani wakati akicheza seti ya pili na kujikuta akishindwa lakini alijikusanya upya kabla ya kuukabili umma wa mashabiki waliokusanyika uwanjani hapo na vyombo vya habari mbali mbali vya dunia.

Lisicki alimshinda bingwa mtetezi Serena Williams na makamu bingwa wa mwaka jana Agnieszka Radwanska katika njia yake kuelekea katika fainali, na alipigiwa upatu kumshinda Bartoli aliyeko katika nafasi ya 15 ya orodha ya wachezaji bora duniani.

Sabine Lisicki of Germany reacts during her women's singles final tennis match against Marion Bartoli of France at the Wimbledon Tennis Championships, in London July 6, 2013. REUTERS/Toby Melville (BRITAIN - Tags: SPORT TENNIS)
Sabine Lisicki Wimbledon Finale 2013Picha: Reuters

Patashika nyingine

Leo Jumapili ( 07.07.2013) mashabiki wa mchezo wa tennis watarejea tena katika viwanja vya Wimbledon kushuhudia fainali ya wanaume, ambapo Novak Djokovic anapambana na Andy Murray katika fainali.

epa03776928 Novak Djokovic of Serbia celebrates a winner against Juan Martin Del Potro of Argentina during their semi-final match for the Wimbledon Championships at the All England Lawn Tennis Club, in London, Britain, 05 July 2013. EPA/KERIM OKTEN +++(c) dpa - Bildfunk+++
Wimbledon Championships 2013 Novak DjokovicPicha: picture-alliance/dpa

Kwa mara ya tatu katika Grand slam nne vijana hao wawili waliozaliwa karibu wakitofautiana kwa wiki moja watatiana kifuani kuwania taji hilo muhimu katika mchezo wa Tennis.

Mwandishi: Sekione Kitojo / rtre / afpe