1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Zanzibar: Wajumbe wa chama cha CUF watoka nje ya Kikao

10 Oktoba 2012

Wajumbe wa baraza la wawakilishi wa CUF mshirika katika serikali ya mapinduzi ya Zanzibar leo (10.10.2012) walitoka nje ya kikao wakati wa kuapishwa mwakilishi mpya wa jimbo la Bububu.

https://p.dw.com/p/16NDM
Wananchi wa chama cha CUF
Wananchi wa chama cha CUFPicha: AP

Uchaguzi huo ulielezwa na chama CUF pamoja na baadhi ya waangalizi kuwa ulijaa matumizi ya nguvu na udanganyifu. CUF ilikwishasema kwamba haitompa ushirikiano mbunge huyo na tayari imepeleka hoja ya kupinga matokeo mahakamani. Sudi Mnette alizungumza na mwandishi wetu kutoka Zanzibar Salma Said ambaye kwanza anasimulia jinsi hali ilivyokuwa kuhusiana na kutoka barazani kwa wawakilishi hao wa chama cha CUF.

(Kusikiliza mazungumzo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini)

Mwandishi: Sudi Mnette

Mhariri:Mohammed Abdul-Rahman