1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BAGHDAD: Mripuko wa bomu Iraq umeua watu 25

22 Mei 2007
https://p.dw.com/p/CBzc

Hadi watu 25 wameuawa na kama 60 wengine wamejeruhiwa katika mripuko wa bomu uliotokea mji mkuu wa Iraq,Baghdad.Watoto wengi ni miongoni mwa wahanga wa shambulizi hilo.Kwa mujibu wa polisi, bomu lililotegwa ndani ya gari liliripuliwa katika soko lililojaa watu katika mtaa wa Amil mjini Baghdad,ambako wakazi wengi ni wa madhehebu ya Kishia.