1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BEIJING: Waziri mkuu wa Japan ziarani China

8 Oktoba 2006
https://p.dw.com/p/CD4v

Waziri mkuu mpya wa Japan,Shinzo Abe amewasili China.Abe ni waziri mkuu wa kwanza wa Japan kuitembelea China tangu miaka mitano ya nyuma.Lengo la ziara yake ni kupunguza mivutano kati ya madola hayo mawili makuu,yenye uchumi mkubwa kabisa barani Asia.Siku ya Jumatatu,Abe ataelekea Korea ya Kusini huku wasi wasi ukizidi kuhusu Korea ya Kaskazini ambayo juma lililopita ilitishia kujaribu bomu lake la kwanza la kinuklia.Kwa maoni ya viongozi wa China na Japan,serikali ya Pyongyang inaweza kufanya jaribio hilo wakati wo wote ule.