1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

GAZA CITY : Kamanda wa Hamas auwawa

21 Novemba 2006
https://p.dw.com/p/CCqi

Vikosi vya Israel vimempiga risasi na kumuuwa kamanda wa kundi la Hamas wakati vilipojipenyeza kwenye mji wa Gaza.

Kwa mujibu wa mashahidi wa Kipalestina mwanamke wa Kipalestina mwenye umri wa miaka 70 pia aliuwawa katika mashambulizi hayo ya Israel.Tukio hilo limekuja masaa machache kufuatia shambulio la Israel kwenye gari katika mji huo wa Gaza ambapo wanamgambo wawili wa Hamas waliuwawa na watu wengine kadhaa kujeruhiwa.

Baada ya shambulio hilo la leo wanamgambo wa Kipalestina walifyatuwa maroketi mawili kwenye mji wa Israel wa Sderot na kumjeruhi vibaya mtu mmoja.

Israel imekuwa ikizidisha mashambulizi yake ya kijeshi ya hivi sasa katika Ukanda wa Gaza kwa jaribio la kukomesha mashambulizi ya maroketi ya Wapalestina ambapo mwanamke mmoja wa Israel ameuwawa wiki iliopita kutokana na mashambulizi hayo ya maroketi.