1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

KABUL: Wanajeshi 2 wa NATO wauawa.

7 Juni 2007
https://p.dw.com/p/CBuK

Askari wawili wa Majeshi ya NATO wameuawa wakati wa makabiliano kati ya majeshi hayo na wanamgambo kusini mwa Afghanistan:

Taarifa ya majeshi hayo imesema askari hao waliuawa jana katika maeneo tofauti wakati majeshi yakipambana na wanamgambo.

Uraia wa wanajeshi hao haujatangazwa .

Mwaka huu pekee, wanajeshi sabini na tisa wameuawa nchini Afghanistan.