LONDON: Washukiwa wa ugaidi wakamatwa Uingereza
10 Mei 2007Matangazo
Watu wanne, akiwemo mjane wa mtu aliyeongoza mashambulio ya bomu ya Julai mwaka 2005, wamekamatwa kuhusiana na mashambulio hayo nchini Uingereza.
Watu hao wanne wanashukiwa kwa mipango ya kutekeleza, kuandaa na kuchochea vitendo vya kigaidi.
Polisi wamewakamata watu hao baada ya msako katika maeneo ya West Yorkshire na Midlands.
Washukiwa hao waliohojiwa na wachunguzi wa shirika la upelelezi la Scotland Yard kuhusiana na mashambulio ya bomu ya Julai Saba, mwaka 2005 dhidi ya vyombo vya usafiri mjini London.
Kiasi watu hamsini na wawili walifariki na wengine mia saba wakajeruhiwa kwenye tukio hilo.