1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Medvedev ataka usalama uimarishwe Urusi

Thelma Mwadzaya25 Januari 2011

Uongozi nchini Urusi umeeleza kuwa mlipuaji wa kujitoa muhanga ndiye aliyesababisha mlipuko katika uwanja mkubwa zaidi wa ndege mjini Moscow.

https://p.dw.com/p/102NJ
Mtu aliyejeruhiwa katika shambulio la uwanja wa DomodedovoPicha: AP

Kiasi ya watu 35 waliuawa na wengine 150 wamejeruhiwa katika shambulio hilo.Kwa mujibu wa msemaji wa uwanja wa ndege wa Domodyedova,mlipuko huo ulitokea kwenye ukumbi wanakowasili maelfu ya abiria wa kimataifa.Muda mfupi baada ya mkasa huo,rais wa Urusi Dmitry Medvedev alimuru usalama uimarishwe katika vituo vyote vya usafiri nchini humo na akaahidi kuwa wahalifu waliohusika watakamatwa. Hata hivyo,mpaka sasa hakuna kundi lolote lilokiri kuhusika na shambulio hilo ijapokuwa mji mkuu wa Urusi wa Moscow umekuwa kwa miaka mingi, shabaha ya wapiganaji wa kiislamu wanaotokea eneo la milima ya Kaskazini.

Domodedowo Moskau Flughafen Anschlag
Magari ya kutoa huduma za dharuraPicha: AP

Mwandishi:Thelma Mwadzaya

Mpitiaji:Hamidou Oummilkheir