1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Waziri Mkuu mpya wa Jordan kutangazwa leo

22 Novemba 2007
https://p.dw.com/p/CRtj

Waziri mkuu wa Jordan,Marouf al-Bakhit amejiuzulu baada ya kumalizika kwa mamlaka ya baraza lake la mawaziri 26 kufuatia uchaguzi wa bunge.Mfalme Abdallah wa Pili anatazamiwa kumteua waziri wa zamani wa usafiri,Nader al-Dahabi kumrithi al-Bakhit.Waziri Mkuu mpya atatangazwa baadae leo hii,Mflame Abdallah atakaporejea nyumbani kutoka ziara yake ya nchini Misri.