1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Waziri Mkuu wa kike wa kwanza Denmark

Martin,Prema/zpr16 Septemba 2011

Chama cha Social Demokrat na vyama shirika vinaongoza kwa wingi mdogo, baada ya takriban kura zote kuhesabiwa katika uchaguzi wa bunge uliofanyika hapo jana nchini Denmark.

https://p.dw.com/p/Rlvl
epa02917473 Helle Thorning-Schmidt, leader of the Danish Labour Party leaves a voting booth to cast her vote in a ballot station in Copenhagen, Denmark, 15 September 2011. Polling stations opened on 15 September 2011 in Danish parliamentary elections called three weeks ago by Prime Minister Lars Lokke Rasmussen. Rasmussen was seeking a fourth term for his centre-right minority government, which has ruled since 2001 with the external backing of the Danish People's Party. Under law, the elections were to be held no later than November. EPA/ERIK REFNER **DENMARK
Mwenyekiti wa chama cha Social Demokrat, Helle Thorning-SchmidtPicha: picture alliance/dpa

Ionekanavyo, mwenyekeiti wa chama cha Social Demokrat, Helle Thorning-Schmidt atakuwa mwanamke wa kwanza kushika wadhifa wa waziri mkuu nchini Denmark. Thorning- Schmidt amejitangaza mshindi wa uchaguzi huo.

Waziri Mkuu wa sasa, Lars Leokke Rasmussen amekiri kuwa ameshindwa na amesema baraza la mawaziri litavunjwa. Chama cha Kiliberali cha Rasmsussen kinachoelemea mrengo wa kulia na chama cha wahafidhina vilitawala Denmark kwa takriban miaka kumi kwa wingi mdogo na kimeungwa mkono bungeni na Chama cha Umma chenye sera kali za mrengo wa kulia. Chama hicho kimeshinikiza sera kali za kudhibiti uhamiaji.