1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wulff atoa wito wa uvumilivu wa kidini

Sekione Kitojo20 Oktoba 2010

Rais wa Ujerumani Christian Wulff kwa mara ya kwanza amehutubia bunge la Uturuki

https://p.dw.com/p/PiQJ
Rais wa Ujerumani Christian Wulff akihutubia katika bunge la Uturuki jana (19.10.2010)Picha: picture alliance/dpa

Ankara.

Rais  wa  Ujerumani  Christian  Wulff  ametoa  wito  wa uvumilivu  zaidi  wa  kidini   katika  hotuba  yake  katika bunge  la  Uturuki . Katika  hotuba  yake  mjini  Ankara , ikiwa  ya  kwanza  kwa  kiongozi  wa  taifa  kutoka Ujerumani, Wulff  amesema   kuwa  ni  muhimu  kuruhusu waumini  wa  dini  ambao  ni  wachache  nchini  Uturuki  na Ujerumani  kuabudu  dini  zao. Wulff  pia  ametumia hotuba  hiyo  ya  kihistoria   kusifu  ushirikiano  baina  ya nchi  hizo  mbili, na  kushughulikia  mjadala  unaoendelea nchini  Ujerumani   kuhusiana  na  ujumuisho  wa Waturuki. Amesisitiza   kuwa  wahamiaji  wa  Kituruki   ni sehemu  ya  Ujerumani, na  kwamba  hawana  haja  ya kupoteza  utambulisho  wao. Ameongeza   hata  hivyo, kuwa  kuna  matatizo  mengi  yanayokabili  ujumuisho wao. Ametoa  wito  kwa   wahamiaji  wote  wa  Kituruki kujifunza  Kijerumani, kufuata  sheria  muhimu,  na kukubali  maadili  ya  kuishi  ya  Kijerumani.