1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Pande hasimu Sudan zilikutana kwa siri mara tatu Bahrain

1 Februari 2024

Viongozi waandamizi wa jeshi la Sudan na wanamgambo wa RSF walikutana mara tatu mwezi uliopita wa Januari huko Bahrain, ikiwa ni mara ya kwanza pande hizo hasimu zinakutana katika kipindi cha miezi tisa ya mapigano.

https://p.dw.com/p/4buRc
Khartoum, Sudan 2019 | Wanamgambo wa RSF
Wanamgambo wa RSFPicha: Hussein Malla/AP Photo/picture alliance

Haya yamesemwa na vyanzo vinavyofahamu mazungumzo hayo. Kulingana na vyanzo hivyo vinne, ambapo viwili vilikuwa kwenye mazungumzo hayo, mikutano hiyo ya Manama ilihudhuriwa manaibu wakuu wenye ushawishi kutoka pande zote mbili na maafisa kutoka Misri na Umoja wa Falme za Kiarabu.

Mazungumzo hayo ambayo hayakutangazwa, yalihudhuriwa pia na maafisa wa Marekani na Saudi Arabia.

Soma pia:Pande zinazozozana za Sudan zinafanya uhalifu Darfur-ICC

Haya yanafanyika wakati ambapo kumekuwa na majaribio ya mara kadhaa ya nchi hizo na hata mataifa ya Afrika Mashariki kujaribu kutafuta suluhu la mzozo huona kusitishwa kwa mapigano.