LONDON:Tetemeko la ardhi lazusha taharuki
28 Aprili 2007Matangazo
Tetemeko la ardhi limeutikisa mji wa Folkestone huko kusini mashariki mwa Uingereza hii leo.
Tetemeko hilo la ardhi kwa mujibu wa polisi limezusha taharuki kubwa kwa wakaazi wa mji huo huku nguvu za umeme zikitatizwa na majumba kadhaa kuharibiwa.
Wanagiologia wa Marekani wamesema tetemeko hilo lilikuwa na kipimo cha richta kati ya 4.7 hadi 5.4
Hata hivyo lakini Treni za chini kwa chini katika eneo hilo ziliweza kufanya kazi kama kawaida.