Wanyarwanda wanaendelea kumiminika katika vituo vya kupigia kura hii leo ili kumchagua rais wao kwa miaka mingine saba// Nchini Kenya kampeni za uchaguzi zinakamilika rasmi kesho Jumamosi zitakaposalia saa 48 kabla raia kupiga kura hapo Jumanne// Tanzania- Habari kutoka jijini Dar es Salaam zinasema kuwa Mahakama Kuu imetupilia mbali zuio la wabunge wanane wa kuteuliwa wa Chama cha Wananchi, CUF.