Baadhi ya wasichana au wanawake hukumbwa na ugumba, hali inayowaacha wakisononeka maishani mwao. Katika makala ya Afya Yako Thelma Mwadzaya anaangazia aina ya hali inayosababisha ugumba kwa wanawake. Kwa lugha ya kitaalamu, huitwa Mayer-Rokitansky-Kuster-Hauser (MRKH). Je wanaojikuta kuwa na hali hiyo huathirika vipi? Changamoto ni zipi? Na je huweza kusuluhishwa?