1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BAGHDAD: Mmuagiko wa damu unaendelea nchini Irak

12 Novemba 2006
https://p.dw.com/p/CCtM

Mashambulio ya bomu leo hii yamesababisha tena mmuagiko mkubwa wa damu nchini Irak.Katika shambulio moja la kujitolea muhanga lililofanywa magharibi mwa mji mkuu Baghdad,kwenye kituo cha polisi cha kuandikisha kazi,watu 34 waliuawa na si chini ya 60 wamejeruhiwa.Shambulio jingine la bomu lililotegwa kando ya barabara na kuwalenga polisi waliokuwa wakipiga doria mashariki mwa Baghdad,liliwaua wapita njia wanne wa Kiiraki na mmoja alijeruhiwa.