1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BAGHDAD: Waziri wa ulinzi wa Marekani afanya ziara ya ghafula Iraq

16 Juni 2007
https://p.dw.com/p/CBrJ

Waziri wa ulinzi wa Marekani,Robert Gates amewasili mji mkuu wa Iraq,Baghdad kwa ziara ya ghafula na amekutana na makamanda wa majeshi ya Marekani.Alipozungumza na waandishi wa habari, Gates alisema,hakuridhika na utendaji kazi wa serikali ya Waziri Mkuu Nouri al-Maliki.Waziri Gates anatazamiwa kumuhimiza al-Maliki kujitahidi zaidi kuleta upatanisho kati ya jamii hasimu na kukomesha machafuko ya kimadhehebu na kushauri kuwa jamii zote zinufaike na mauzo ya mafuta.