1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BAGHDAD.Kituo cha televisheni cha Wassuni chavamiwa

12 Oktoba 2006
https://p.dw.com/p/CD3X

Watu wenye silaha wamezivamia afisi za kituo cha matangazo ya televisheni kwa satellite mjini Baghdad na kuwauwa walinzi na wafanyakazi kiasi wanne.

Ripoti zinasema kwamba hujuma hiyo ilifanywa mapema leo asubuhi.

Kituo hicho cha televisheni cha Saabia ni cha Wassuni, hali inayoashiria huenda mauaji hayo yanahusiana na uhasama kati ya Wassuni na Washia.

Hakuna taarifa zaidi zilizopatikana.