1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BAGHDAD:watu 27 zaidi waangamia nchini Irak

23 Agosti 2007
https://p.dw.com/p/CBWn

Watu wasiopungua 27 wameuawa katika shambulio la kujitoa mhanga kwenye mji wa Beiji kaskazini mwa Irak.

Watu wengine kadhaa walijeruhiwa katika shambulio hilo ambapo mshambuliaji alilitosa lori lake katika kituo cha polisi na kulipua mabomu.

Habari zaidi zinasema kuwa wengi wa waliouawa walikuwa raia.

Wakati huo huo askari 14 wa Marekani wameuawa baada ya helikpota yao kuanguka kaskazini mwa Irak.